Kitendo cha Juma Nature kumkejeli na kumdhihaki Diamond ni ishara ya wivu

Joined
Mar 14, 2026
Messages
33,422
JF....!

Hivi sasa kuna wimbo mpya wa msanii Juma Nature feat Jay Dee unaioitwa "kama jana" wimbo huu ni mzuri sana pia una maudhui mazuri ya kuwahasa wasanii kufanya mziki kiubunifu kama wa bongo flava ya zamani ambao ulidumu.


Lakini kilichonisikitisha ni verse ya Juma nature ambapo kuna maneno ya kumdhihaki na kumkejeli msanii Diamond Platinumz kuwa mkata mauno na limbukeni wa umaarufu" hali hii imenifanya nijulize maswali mengi kama Nature aliwaza nini hadi kuimba hivyo? Au ndiyo kusema huu ni muendelezo wa fustration za wasanii wa zamani baada ya kuona mziki wao umezidiwa soko na vijana wa sasa wanaochipukia?


 
 
Back
Top Bottom