- Joined
- Mar 14, 2026
- Messages
- 33,422
Benki Kuu imetoa ripoti yake kwa ajili ya mwaka wa fedha 2007/2008 ambayo inaonyesha deni la Taifa kuongezeka kwa takriban 25% katika mwaka mmoja! Deni letu la nje bado ni kubwa ingawa deni la ndani linapungua.
Deni hili la Taifa ni 33% ya GDP ya nchi.
Je deni hili linaloongezeka kila siku ni nani atalilipa na ni lini litalipwa?
Ama ni kwa nini deni hili linalongezeka kutokana na kuendelea kukopa na riba itokanayo na mikopo ambayo tayari bado iko katika vitabu na majedwali ya mapato na matumizi ya nchi yetu?
Nimetatizwa sana na kauli ya Naibu Waziri wa Fedha Jeremiah Sumari ambaye amedai kuwa tusiwe na shaka kuhusu kuongezeka kwa deni hili na ni deni ambalo tunaweza kulihimili na kulilipa! Zaidi ni kitendo cha Sumari kudai kuwa kuna nchi nyingine ambazo zina uwiano mkubwa wa Deni lao la Taifa kuliko Tanzania hivyo hakuna haja ya kuogopa!
Je wewe Mtanzania mwenzangu unaipokeaje kauli hii ya kusema usiwe na wasiwasi tunaendelea kukopa huku hali halisi ni kuwa hatuna nguvu za kiuzalishaji mali na ukusanyaji mapato ambazo zitalipa Taifa pato la kuweza kujitegemea na kupunguza mzigo huu wa kutegemea mikopo na misaada kujiendesha?
Kama unaridhika na kauli ya Sumari, basi nakwambia wazi kuwa wewe utaendelea kuwa masikini na ombaomba na kamwe hutaweza kujitutumua na kujitegemea.
Kama umeshikwa na hasira kama Mchungaji ya kusikia kauli hasi kutoka kwa kiongozi mkubwa kama huyu, basi itakulazimu ujiulize ni vipi tunaendelea kukopa na hata kuongeza deni na ni nani anayetuongezea mzigo huu wa deni hili!
Je ni wewe Mtanzania au ni Viongozi ambao wamekosa mwamko wa kujenga uchumi unaojitegemea?
Tunapofikia mahali tunajigamba kuwa deni letu ni bora kuliko la Rwanda, Kenya hata Msumbiji, tujiulize je nao wana rasilimali sawa na zetu? Je uzalishaji mali wetu wa ndani ni sawa? Je mikopo na deni ni kutokana na matumizi sawa na kimaendeleo?
Nina uhakika kwa asilimia 85% kuwa sehemu kubwa ya mikopo (70%) imetumika kwa matumizi yasiyo ya lazima na yangeweza kupunguzwa.
Cha kutisha ni kuwa Tanzania si kwamba haina fedha wala uwezo wa kujitegemea, bali ni mazoea mabaya ya kukopa ambayo yamejenga mizizi mibaya inayoeta uzembe na hata ufisadi na hivyo dhana ya kuwa wabanifu na kutumia kwa uangalifu tulicho nacho haiko tena.
Tatizo kubwa la Serikali ya Tanzania ni matumizi yasiyo na kikomo wala kuwa na hamasa ya kubana matumizi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima au kama wenzetu wanavyoyaita Wasteful spending!
Mfano wa matumizi yasiyo na faida wala manufaa ni Serikali kung'ang'ania kuwa mshiriki wa uzalishaji mali katika sekta ambazo kuna ushindani tosha wa sekta binafsi. Hili husababisha kuanzishwa kwa mashirika, taasisi na miradi ambayo inaweza kufanya na watu binafsi na Serikali wajibu wake uwe ni kwenye uratibu.
La zaidi katika matumizi mabovu na yasiyo ya lazima ni kule kuhalalisha vitu ambavyo vinaweza kufanywa kwa kutumia teknolojia ya simu, barua pepe au watendaji wachache.
Mfano, kuna tabia kubwa ya kukimbilia kuandaa makongamano, semina, warsha na hata mikutano isiyo na ulazima ambayo hutumia fedha nyingi za walipa kodi na kudonoa fungu la misada na mikopo ambalo lilipaswa kutumika kwa miradi ya kimaendeleo na kuishia kuwa matumizi ya kawaida. Kwenye hivi vikao, kuna malipo ya usafiri na malazi, kushiriki kikao na mengineyo kwa ajili ya watu ambao hulipwa mishahara kwa kufanya kazi ambazo ni wajibu wao.
Ama misafara ya kila mtu inapofika mahali kiongozi anafanya ziara ya kutembelea sehemu, utakuta kuna zaidi ya watu 100 ambao kazi yao ni upambe kwa kudai eti wanapaswa kuandamana na kiongozi.
Sasa matumizi kama haya, yanaipunguzia Serikali mapato ukiongezea uzalishaji mali wetu ulio duni na wa kijima ambao hauna uwezo imara kusimama kidete katika ushindani wa kimataifa.
Rushwa na Takrima nayo ni mchangiaji mkubwa wa kukua kwa deni letu. Mwaka 2007, asilimia 20% ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya Bajeti zilipotea katika mazingira ya rushwa. Mwaka uliofuatia, Rushwa katika ufujaji wa bajeti uliongezeka kwa asilimia 10% hivyo kufanya upotevu wa Bajeti katika miaka miwili kuwa asilimia 50%!
Sasa kama tunapoteza mapato na kufuja hazina yetu kwa kiwango hiki, iweje Sumari atuambie tusiwe na wasiwasi tunapoona deni la Taifa linaongezeka?
Ninauliza ni nani atalilipa deni hili huku hata uzalishaji mali ni duni, rasilimali tunazitapanya na mapato kupitia kodi ni madogo kutokana na kutoa misamaha ya kodi na ukosefu wa uhakiki wa mapato ya wawekezaji?
Kama tungepunguza matumizi na mfumuko wa deni, tungeongeza kipato cha Mtanzania hata kwa asilimia 25% ya kima cha chini, hii ni zaidi ya shughuli nyingine za maendeleo na ulazima kama elimu, afya, miundombinu na hata nishati.
Kauli ya Sumari inanifanya niamini kuwa kamwe kama hatuta leta mabadiliko ya kweli ndani ya mfumo wetu wa kisiasa na utendaji kazi na maendeleo, tutaendelea kujilundikia madeni.
Sumari katuambia, pondamali kufa kwaja, je nawe wakubali hilo? Mwanao na mjukuu wataishije?
Deni hili la Taifa ni 33% ya GDP ya nchi.
Je deni hili linaloongezeka kila siku ni nani atalilipa na ni lini litalipwa?
Ama ni kwa nini deni hili linalongezeka kutokana na kuendelea kukopa na riba itokanayo na mikopo ambayo tayari bado iko katika vitabu na majedwali ya mapato na matumizi ya nchi yetu?
Nimetatizwa sana na kauli ya Naibu Waziri wa Fedha Jeremiah Sumari ambaye amedai kuwa tusiwe na shaka kuhusu kuongezeka kwa deni hili na ni deni ambalo tunaweza kulihimili na kulilipa! Zaidi ni kitendo cha Sumari kudai kuwa kuna nchi nyingine ambazo zina uwiano mkubwa wa Deni lao la Taifa kuliko Tanzania hivyo hakuna haja ya kuogopa!
Je wewe Mtanzania mwenzangu unaipokeaje kauli hii ya kusema usiwe na wasiwasi tunaendelea kukopa huku hali halisi ni kuwa hatuna nguvu za kiuzalishaji mali na ukusanyaji mapato ambazo zitalipa Taifa pato la kuweza kujitegemea na kupunguza mzigo huu wa kutegemea mikopo na misaada kujiendesha?
Kama unaridhika na kauli ya Sumari, basi nakwambia wazi kuwa wewe utaendelea kuwa masikini na ombaomba na kamwe hutaweza kujitutumua na kujitegemea.
Kama umeshikwa na hasira kama Mchungaji ya kusikia kauli hasi kutoka kwa kiongozi mkubwa kama huyu, basi itakulazimu ujiulize ni vipi tunaendelea kukopa na hata kuongeza deni na ni nani anayetuongezea mzigo huu wa deni hili!
Je ni wewe Mtanzania au ni Viongozi ambao wamekosa mwamko wa kujenga uchumi unaojitegemea?
Tunapofikia mahali tunajigamba kuwa deni letu ni bora kuliko la Rwanda, Kenya hata Msumbiji, tujiulize je nao wana rasilimali sawa na zetu? Je uzalishaji mali wetu wa ndani ni sawa? Je mikopo na deni ni kutokana na matumizi sawa na kimaendeleo?
Nina uhakika kwa asilimia 85% kuwa sehemu kubwa ya mikopo (70%) imetumika kwa matumizi yasiyo ya lazima na yangeweza kupunguzwa.
Cha kutisha ni kuwa Tanzania si kwamba haina fedha wala uwezo wa kujitegemea, bali ni mazoea mabaya ya kukopa ambayo yamejenga mizizi mibaya inayoeta uzembe na hata ufisadi na hivyo dhana ya kuwa wabanifu na kutumia kwa uangalifu tulicho nacho haiko tena.
Tatizo kubwa la Serikali ya Tanzania ni matumizi yasiyo na kikomo wala kuwa na hamasa ya kubana matumizi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima au kama wenzetu wanavyoyaita Wasteful spending!
Mfano wa matumizi yasiyo na faida wala manufaa ni Serikali kung'ang'ania kuwa mshiriki wa uzalishaji mali katika sekta ambazo kuna ushindani tosha wa sekta binafsi. Hili husababisha kuanzishwa kwa mashirika, taasisi na miradi ambayo inaweza kufanya na watu binafsi na Serikali wajibu wake uwe ni kwenye uratibu.
La zaidi katika matumizi mabovu na yasiyo ya lazima ni kule kuhalalisha vitu ambavyo vinaweza kufanywa kwa kutumia teknolojia ya simu, barua pepe au watendaji wachache.
Mfano, kuna tabia kubwa ya kukimbilia kuandaa makongamano, semina, warsha na hata mikutano isiyo na ulazima ambayo hutumia fedha nyingi za walipa kodi na kudonoa fungu la misada na mikopo ambalo lilipaswa kutumika kwa miradi ya kimaendeleo na kuishia kuwa matumizi ya kawaida. Kwenye hivi vikao, kuna malipo ya usafiri na malazi, kushiriki kikao na mengineyo kwa ajili ya watu ambao hulipwa mishahara kwa kufanya kazi ambazo ni wajibu wao.
Ama misafara ya kila mtu inapofika mahali kiongozi anafanya ziara ya kutembelea sehemu, utakuta kuna zaidi ya watu 100 ambao kazi yao ni upambe kwa kudai eti wanapaswa kuandamana na kiongozi.
Sasa matumizi kama haya, yanaipunguzia Serikali mapato ukiongezea uzalishaji mali wetu ulio duni na wa kijima ambao hauna uwezo imara kusimama kidete katika ushindani wa kimataifa.
Rushwa na Takrima nayo ni mchangiaji mkubwa wa kukua kwa deni letu. Mwaka 2007, asilimia 20% ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya Bajeti zilipotea katika mazingira ya rushwa. Mwaka uliofuatia, Rushwa katika ufujaji wa bajeti uliongezeka kwa asilimia 10% hivyo kufanya upotevu wa Bajeti katika miaka miwili kuwa asilimia 50%!
Sasa kama tunapoteza mapato na kufuja hazina yetu kwa kiwango hiki, iweje Sumari atuambie tusiwe na wasiwasi tunapoona deni la Taifa linaongezeka?
Ninauliza ni nani atalilipa deni hili huku hata uzalishaji mali ni duni, rasilimali tunazitapanya na mapato kupitia kodi ni madogo kutokana na kutoa misamaha ya kodi na ukosefu wa uhakiki wa mapato ya wawekezaji?
Kama tungepunguza matumizi na mfumuko wa deni, tungeongeza kipato cha Mtanzania hata kwa asilimia 25% ya kima cha chini, hii ni zaidi ya shughuli nyingine za maendeleo na ulazima kama elimu, afya, miundombinu na hata nishati.
Kauli ya Sumari inanifanya niamini kuwa kamwe kama hatuta leta mabadiliko ya kweli ndani ya mfumo wetu wa kisiasa na utendaji kazi na maendeleo, tutaendelea kujilundikia madeni.
Sumari katuambia, pondamali kufa kwaja, je nawe wakubali hilo? Mwanao na mjukuu wataishije?