Kuanzisha Biashara

Joined
Mar 14, 2026
Messages
33,422
Wana JF

Katika pitapita zangu ndani ya jukwaa hili nimejionea mambo mengi sana ambayo yanaweza kutusaidia kama Watanzania kujikwamua kiuchumi.


Pamoja na hayo mimi pia nimefika mahali nimeona ni bora na mimi niombe ushauri wa jinsi ya kuanzisha biashara ili angalau niweze kukuza kipato changu kwani kwa kutegemea ajira siyo rahisi mafanikio ya kiuchumi kupatikana. Mimi ni mhandisi na ningependa kumiliki kampuni ya Uzabuni (Contractor) itakayojihusisha zaidi na masuala ya umeme & Mitambo (electrical & mechanical) ila ugumu ninaouona ni suala zima la utaratibu na pia mahitaji muhimu kwa biashara hii sana sana vitu kama mtaji na rasilimali zingine.


Kwa wana JF wenzangu naamini kabisa wapo wenye upeo mkubwa juu ya hili, naombeni mnipe ushauri wa nini naweza kufanya ili kuitimiza adhma yangu ya kumiliki biashara yangu mwenyewe. Pia kama kuna ideas zingine nitashukuru kama mtanipatia


Nawasilisha...


 
 
Back
Top Bottom